Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi za ‘kimapinduzi’ kuanza kuunguruma
Habari Mchanganyiko

Kesi za ‘kimapinduzi’ kuanza kuunguruma

Spread the love

KESI za kupinga watuhumiwa kukamatwa kabla ya upelelezi kukamilika, pamoja na kunyimwa haki ya dhamana inaanza kutajwa leo tarehe 13 Februari 2020. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Kesi hizo zilizofunguliwa na Wanaharakati wa Haki za Binadamu nchini Tanzania, katika Mahakama Kuu ya Dar es Salaam.

Kesi ya kwanza Na. 35/2019, imefunguliwa na Paul Kisabo, Mwanasheria wa Mtandao wa Watetetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kupinga watuhumiwa wa makosa ya uhujumu uchumi kunyimwa dhamana.

Kesi hiyo inatarajiwa kutajwa kwa mara ya kwanza leo tarehe 13 Februari 2020 mbele ya majaji watatu, Jaji  Dk.Benhajj Masoud, Jaji Magoiga na Jaji Juliana Masabo.

Kesi ya pili Na. 36/2019 imefunguliwa Onesmo Olengurumwa, Mratibu wa Kitaifa wa THRDC, inayopinga watuhumiwa wa makosa mbalimbai kufikishwa kwenye mahakama zisizokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi zao.

Pia, Olengurumwa anapinga watuhumiwa wa makosa mbalimbali kukamatwa bila ya upelelezi kukamilika.

Kesi hiyo pia inatarajiwa kutajwa leo mbele ya majaji watatu, Jaji Benhajj Masoud, Jaji Mlyambina na Jaji Juliana Masabo.

Katika kesi hiyo, Olengurumwa anaiomba mahakama hiyo kutoa tamko la kufuta vifungu vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20, kw amadai kwmaba vinakiuka haki na uhuru wa watuhumiwa, kuminya utawala wa sheria  pamoja na kufifisha mchakato wa uendeshaji kesi kwa usawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!