Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tume Huru: Wazee Chadema ‘tatizo si Magufuli, ni Kikwete’
Habari za Siasa

Tume Huru: Wazee Chadema ‘tatizo si Magufuli, ni Kikwete’

Hashim Juma, Mwenyekiti wa BAZECHA
Spread the love

BAZARA la Wazee la Chama cha Chadema (BAZECHA), limesema mkwamo Tume wa Huru ya Uchaguzi, umesababishwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 13 Januari 2020, jijini Dar es Salaam, Hashim Juma, Mwenyekiti wa BAZECHA amesema, Rais Kikwete anastahili lawama kutokana na kupuuza Rasimu ya Katiba ya Jaji Mstaafu, Joseph Warioba, iliyopendekeza uundwaji wa tume hiyo.

Amedai, baada ya Rais Kilwete kugundua Katiba hiyo imeweka vipengele vinavyombana rais, alimshauri Rais Magufuli kuachana na mchalato huo, ili rasimu hiyo isifanyiwe kazi.

“Tusimlaumu sana, kweli ana makosa yake lakini wa kumlaumu Kikwete (Rais Kikwete) sababu tume iliundwa, ikatumiwa mabilioni lakini mwisho wa siku alivyoona, tume inataka kuleta Tume Huru ya Uchaguzi na rais kupingwa, akaipiga chini.

“…na wakamuelekeza Magufuli (Rais Magufuli) kuipuuza Katiba Mpya. Wakati anaingia madarakani alisema, ataiendeleza baada ya kuingia madarakani akageuka akasema sio kipaumbele chake,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

error: Content is protected !!