Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tume Huru: Wazee Chadema ‘tatizo si Magufuli, ni Kikwete’
Habari za Siasa

Tume Huru: Wazee Chadema ‘tatizo si Magufuli, ni Kikwete’

Hashim Juma, Mwenyekiti wa BAZECHA
Spread the love

BAZARA la Wazee la Chama cha Chadema (BAZECHA), limesema mkwamo Tume wa Huru ya Uchaguzi, umesababishwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 13 Januari 2020, jijini Dar es Salaam, Hashim Juma, Mwenyekiti wa BAZECHA amesema, Rais Kikwete anastahili lawama kutokana na kupuuza Rasimu ya Katiba ya Jaji Mstaafu, Joseph Warioba, iliyopendekeza uundwaji wa tume hiyo.

Amedai, baada ya Rais Kilwete kugundua Katiba hiyo imeweka vipengele vinavyombana rais, alimshauri Rais Magufuli kuachana na mchalato huo, ili rasimu hiyo isifanyiwe kazi.

“Tusimlaumu sana, kweli ana makosa yake lakini wa kumlaumu Kikwete (Rais Kikwete) sababu tume iliundwa, ikatumiwa mabilioni lakini mwisho wa siku alivyoona, tume inataka kuleta Tume Huru ya Uchaguzi na rais kupingwa, akaipiga chini.

“…na wakamuelekeza Magufuli (Rais Magufuli) kuipuuza Katiba Mpya. Wakati anaingia madarakani alisema, ataiendeleza baada ya kuingia madarakani akageuka akasema sio kipaumbele chake,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!