Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee aweka msimamo Kawe 2020
Habari za Siasa

Mdee aweka msimamo Kawe 2020

Halima Mdee, aliyekuwa ubunge wa Kawe kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

HALIMA Mdee, Mbunge wa Kawe, jijini Dar es Salaam amesema, hakuna wa kumbabaisha kwenye Jimbo la Kawe, kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Mdee ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA) amesisitiza, mtu wa kumng’oa katika Jimbo la Kawe, hajazaliwa.

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Januari 2020, alipoulizwa na MwanaHALISI Online kwamba, inaeleza kuwa na hofu ya kushindwa kwenye jimbo hilo.

Na kwamba, taarifa zinaeleza kuwa hana mpango wa kugombea kwenye jimbo katika uchaguzi mkuu wa 2020, hivyo karata pekee ya kumfanya kuwa mbunge ni kupitia Viti Maalum akiwa Mwenyekiti BAWACHA.

“…mpaka sasa hakuna wa kuniondoa Kawe, hajazaliwa mpaka sasa,” Mdee amesema kwa kifupi akidai, wakati wa kutoa maelezo marefu kuhusu swali hilo, haujafika.

Mdee pia amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutorudia iliyofanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kwamba hakitavumilika tena.

“Wasije wakafikiria uhuni wa serikali za mitaa wataufanya kwenye uchaguzi wa madiwani na wabunge. Kwanza huko chini hakukaliki. Wamejipa vyeo kinadharia lakini vitendo Chadema ndio mpango mzima kitaa,” amesema Mdee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!