Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mama Kabendera aagwa, kuzikwa Jumatatu Bukoba
Habari za Siasa

Mama Kabendera aagwa, kuzikwa Jumatatu Bukoba

Spread the love

MWILI wa Verdiana Mujwahuzi, Mama wa Mwanahabari Erick Kabendera, leo tarehe 3 Januari 2020, umeagwa katika Kanisa Katoliki la Mt. Francis Xavier, Chang’ombe jijini Dar es Salaam. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Wanaharakati mbalimbali, wanasiasa na wananchi wa kawaida, wameshiriki kuuaga mwili wa Mama Kabendera, aliyefariki dunia tarehe 31 Desemba 2019, katika Hospitali ya Amana.

Miongoni mwa watu walioshiriki kumuaga Mama wa Kabendera ni, Anna Henga, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Onesmo Ole- Ngurumwa, Mratibu Mkuu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC).

Wengine ni Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, John Mnyika Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Akitoa salamu za rambirambi kutoka kwa Asasi za Kiraia (AZAKI), Henga amesema Mama Kabendera ameondoka na uchungu wa mwanaye kukaa mahabusu gerezani, na kuahidi kwamba watetezi wa haki za binadamu hawataacha kumtetea Kabendera.

“Tunajua mama anaondoka kwa uchungu juu ya mwanaye na hii inadhihirisha na kauli aliyoitoa kabla ya kufariki. Sisi watetetezi wa haki za binadamu tunahuzunika kwa aliyokutana nayo Erick hata kushindwa kumuaga mama yake.

Tutatoa ahadi tutaendelea kumsaidia kwa msaada wa kisaikolojia na kisheria. Mbele ya mama na madhahabu hii tunaahidi kumsaidia,” ameahizi Henga.

Paul Baregu, Msemaji wa familia ya Kabendera, amesema Mama Mujwahuzi atazikwa siku ya Jumatatu tarehe 6 Januari 2020, nyumbani kwao Bukoba, mkoani Kagera.

Msemaji huyo wa familia amesema kabla ya kifo chake, marehemu alivimba mwili mzima, na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Amana, lakini alifariki dunia kabla majibu ya uchunguzi kutolewa.

“Alisumbuliwa na mwili kuvimba. Alivimba mwili wake wote familia ilimpeka hospitali ya Amana kwa ajili ya uchunguzi. Alifariki dunia kabla ya majibu ya vipimo alivyopimiwa hayajapatikana,” amesema

Akitoa wasifu wa marehemu, Baregu amesema Mama Kabendera alizaliwa mwaka Februari 2 , 1939 mkoani Kagera, ameacha watoto 7 kati ya 8 baada ya mmoja kufariki. Ameacha wajukuu 16 na vitukuu 3.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!