Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM kumweka kikaangoni Mwita Waitara
Habari za SiasaTangulizi

CCM kumweka kikaangoni Mwita Waitara

Mwita Waitara
Spread the love

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Mara kimesema kitamuita kwenye Kamati ya Maadili, Mwita Waitara, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, ili kujibu tuhuma za kuvunja kanuni za uchaguzi za chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza na Wanahabari jana tarehe 3 Januari 2020, Samweli Kiboye, Mwenyekiti wa CCM Mkoani Mara, amesema Waitara amefanya makosa kujinadi kuwa atagombea Jimbo la Tarime Vijijini,  kinyume na katiba ya chama hicho, kwa kuwa kipindi cha uchaguzi bado hakijafika.

“Lazima tutumie kanuni zetu za CCM,  kanuni za uchaguzi, lazima tumwite katika vikao vyetu hatuwezi kumuacha mtu anajinadi. Kwa sababu akishaanza kujinadi ataleta makundi Tarime, tunataka WanaTarime tuikomboe Tarime, tunavyoenda hivi tutaleta makundi,” amesema Kiboye.

Mwenyekiti huyo wa CCM mkoani Mara, amesema Mwita ataitwa kwenye kamati hiyo, ili kujibu utaratibu aliotumia kujitangaza kugombea Ubunge wa Tarime Vijijini.

“Atatueleza ametoa mfumo wake wapi wa kujitangaza, au kama yeye anajiona yuko juu ya chama ndani ya Tarime, asije akatuharibia chama Wilaya ya Tarime,” ameeleza Kiboye.

Kiboye ameonya watu wanaoanza kujinadi kugombea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, akisema kwamba, hatamuogopa mtu yeyote kwa kuwa hakuna mtu aliye juu ya CCM.

“Natoa onyo vikao vitafuata na hatutamuonea mtu haya, hatutamuogopa yeyote awe na cheo kiasi gani, chama ndio kikubwa. Hakuna mtu aliyejuu ya chama, chama ndio bosi uhoji mtu yeyote, lazima tuwahoji tutawaita katika kamati ya maadili,” ameonya Kiboye.

Mwita ambaye ni Mbunge wa Ukonga, hivi karibuni alitangaza kugombea ubunge wa jimbo hilo, na kuahidi kuchuana na John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!