Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Pigo Pwani, Katibu Chadema amfuata Sumaye
Habari za Siasa

Pigo Pwani, Katibu Chadema amfuata Sumaye

Casmir Mabina, Katibu wa Chadema Kanda ya Pwani
Spread the love

MAZINGIRA ya demokrasia goigoi ndani ya Chama cha Demokrasia na Mamendeleo (Chadema), yamemkimbiza Casmir Mabina, Katibu wa Chadema Kanda ya Pwani. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Mabina ametangaza uamuzi huo leo tarehe 4 Desemba 2019, jijini Dar es Salaam, saa chache baada ya Fredrick Sumaye, aliyekuwa mwenyekiti wa kanda hiyo, kutangaza kujiondoa Chadema.

Ingawa hakueleza sababu za kujiuzulu wadhifa huo, Mabina amesema ameamua kujiuzulu kutokana na mazingira ya siasa yaliyokuwepo ndani ya Chadema.

“Kutokana na mazingira ya kisiasa yalivyo ndani ya Chadema, leo nimewasilisha barua yangu ya kujiuzulu. Kwamba kwa mazingira haya lazima nijiuzluzu,” ameeleza Mabina.

Mabina amesema, atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa Chadema.

“Nimeeleza nitabakia kuwa mwanachama wa kawaida katika chama change, kwenye tawi langu. Labda kama kutakuwa na mambo mengine yatakayojitokeza,” amesema Mabina

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

error: Content is protected !!