Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Pambalu ajitosa uenyekiti BAVICHA
Habari za Siasa

Pambalu ajitosa uenyekiti BAVICHA

Bendera ya Chadema
Spread the love

JOHN Pambalu, Diwani Kata ya Butimba jijini Mwanza, ametangaza nia ya kugombea uenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha). Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Pambalu ambaye ni Makamu Mwenyekiti Bavicha, ametangaza nia hiyo leo tarehe 30 Novemba 2019, baada ya kurejesha fomu ya kugombea uenyekiti wa baraza hilo, kwenye Ofisi za Chadema, zilizoko jijini Dar es Salaam.

“Nimeamua kuutangazia umma wa Watanzania na dunia kwa ujumla kwamba, nimetia nia ya kugombea uenyekiti wa Bavicha.  Uamuzi umekuja baada ya kujitafakari kwa ajili ya ukumbozi wetu,” amesema Pambalu.

Pambalu amesema amechukua hatua hiyo, ili kuwakomboa vijana na Watanzania kwa ujumla, kupitia Bavicha.

“Nimejipima nikaona katika siasa hizi za awamu ya tano, zinahitaji kijana jasiri dhidi ya siasa hizi za mabavu. Nina dhamira ya Kutatua changamoto za watanzania kupitia Bavicha, kwa kushirikiana na Chadema,” ameeleza Pambalu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!