Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nasikia naitwa polisi, ngoja niende – Lema
Habari za Siasa

Nasikia naitwa polisi, ngoja niende – Lema

Spread the love

GODBLESS Lema, Mbunge wa Arusha Mjini, leo tarehe 14 Novemba 2019 amesema, amepewa taarifa za wito wa Jeshi la Polisi wilayani Hai, Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

“Polisi wamevamia nyumbani kwa Mwenyekiti wa Halmshauri Hai, Helga Mchomvu, wamemkamata dereva wangu na gari yangu nyumbani kwa Helga, Nimepewa taarifa kuwa, ninatafutwa. Nimeamua kuelekea Kituo cha Polisi Hai,” Lema ameandika kwenye ukurasa wake wa twitter.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, wito wa Lema kwenda polisi umetolewa na Lengai Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai akidai kwenda kufanya njama za vurugu kwenye wilaya yake.

Taarifa zinaeleza, Lema alikuwa Hai kufanya vikao vya ndani vya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), na kwamba vitendo vya wanasiasa kutoka maeneo yao na kwenda maeneo mengine vimezuiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!