Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai ‘anyonga’ swali la Mbunge Chadema
Habari za Siasa

Spika Ndugai ‘anyonga’ swali la Mbunge Chadema

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

SWALI la papo kwa papo Kasim Majaliwa, Waziri Mkuu kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa, ‘limenyongwa’ juu kwa juu na Job Ndugai, Spika wa Bunge. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Devotha Minja, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), wakati akianza kutoa maelezo kuhusu swali lake, Spika Ndugai alimzuia kuendelea kwa maelezo, kanuni za Bunge hazirihuru ‘kuandikiwa swali.’

Leo tarehe 14 Novemba 2019, Minja alianza kutoa maelezo kuhusu hila na hujuma zinazofanywa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mbunge huyo alijikita kwenye kauli zilizotolewa na Seleman Jafo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Mwita Waitara, Naibu Waziri wa TAMISEMI.

Mwelekeo wa swali la Minja kabla ya kuuliza swali lenyewe, ulikiutana na kigingi cha Spika Ndugai, na kujikuta akitupwa nje na nafasi ya kuuliza kupewa mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Hilo swali si lako, umeandikiwa na waliokutuma,” aliambiwa Minja ambaye naye alijibu “sijaandikiwa.”

Spika Ndugai alihama kwa Minja na nafasi hiyo kumpa Allan Kiula,

Mbunge wa Mkalama (CCM), ambaye alijikita katika hofu kuhusu haki ya kupiga na kupigiwa kura katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 24 Novemba 2019.

Hata hivyo, Waziri Majaliwa alisisitiza kuzingatiwa kwa sheria, kanuni na taratibu katika kutimiza azma ya kuchagua viongozi kwenye uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!