Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango: Tusisalimu amri
Habari za Siasa

Dk. Mpango: Tusisalimu amri

Dk. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

DAKTARI Phillip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango amezitaka nchi za Afrika kutosalimu amri, kwa mataifa ya kigeni, yanayohatarisha uhuru wa kujitawala. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Dk. Mpango ametoa kauli hiyo jana tarehe 25 Oktoba 2019, katika Kongamano Maalumu la Vita vya Kiuchumi na Hatma ya Afrika, lililofanyika jijini Dar es Salaam.

“Kamwe tusisalimu amri, kwa wale wanaojaribu kupinda mikono yetu na kuhatarisha uhuru wetu wa kujitawala,” amesema Dk. Mpango.

Waziri huyo wa fedha ameeleza kuwa, nchi za Afrika zimepata uhuru wa kisiasa lakini zimekosa uhuru wa kiuchumi.

“Tumepata uhuru wa kisiasa, lakini uhuru wa kiuchumi bado. Fikra za utegemezi, uhisani bado zipo. Inabidi tuzipige vita. Lakini pili, Afrika lazima izingatie misingi ya usimamizi wa uchumi. Ni lazima nchi zetu tuzielekeze kupanua wigo wa kiuchumi kwa upande wa uzalishaji masoko na mtaji,” amesema Dk. Mpango.

Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema nchi za Afrika zilizoamua kujitegemea ziko vitani kutokana na vitimbi vya mataifa yaliyoendelea.

“Tuko vitani, tunaishi kwenye nchi za vitimbi hasa kwa mataifa yanayoamua kujitegemea,” amesema Prof. Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!