Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Azam FC yatambulisha kocha mpya
Michezo

Azam FC yatambulisha kocha mpya

Aristica Cioaba
Spread the love

KLABU ya Azam FC leo imemtambulisha rasmi, Arastica Cioaba kuwa kocha mkuu wa timu hiyo aliyekuja kuchukua nafasi ya Ettien Ndailagije aliyeiongoza timu hiyo muda mfupi huku akiwa Kocha wa muda wa Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars.” Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Cioaba ambaye ni raia wa Romania ameingia mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha timu hiyo yenye maskani yake Chamazi jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mara ya pili ndani ya miaka miwili.

Aidha kocha huyo mwenye leseni ya juu ya ukocha ya UEFA amerejea sambamba na kocha wa viungo Costel Birsan aliyekuwa naye awali wakati anaifundisha Azam FC.

Ikumbuke hii ni mara ya pili kwa kocha huyo kujiunga na Azam FC, baada ya kufukuzwa hapo awali kutokana na timu kutofanya vizuri katika michuano ya Ligi Kuu na michuano ya kimataifa toka aliposaini mkataba Januari 5, 2017.

Azam kwa sasa itakuwa imefundishwa jumla na makocha kumi toka ilipopanda Ligi Kuu mwaka 2008 na kufanikiwa kutwaa ubingwa mara moja 2014 chini ya kocha Joseph Omog.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!