Saturday , 3 June 2023
Home Kitengo Michezo Azam FC yatambulisha kocha mpya
Michezo

Azam FC yatambulisha kocha mpya

Aristica Cioaba
Spread the love

KLABU ya Azam FC leo imemtambulisha rasmi, Arastica Cioaba kuwa kocha mkuu wa timu hiyo aliyekuja kuchukua nafasi ya Ettien Ndailagije aliyeiongoza timu hiyo muda mfupi huku akiwa Kocha wa muda wa Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars.” Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Cioaba ambaye ni raia wa Romania ameingia mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha timu hiyo yenye maskani yake Chamazi jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mara ya pili ndani ya miaka miwili.

Aidha kocha huyo mwenye leseni ya juu ya ukocha ya UEFA amerejea sambamba na kocha wa viungo Costel Birsan aliyekuwa naye awali wakati anaifundisha Azam FC.

Ikumbuke hii ni mara ya pili kwa kocha huyo kujiunga na Azam FC, baada ya kufukuzwa hapo awali kutokana na timu kutofanya vizuri katika michuano ya Ligi Kuu na michuano ya kimataifa toka aliposaini mkataba Januari 5, 2017.

Azam kwa sasa itakuwa imefundishwa jumla na makocha kumi toka ilipopanda Ligi Kuu mwaka 2008 na kufanikiwa kutwaa ubingwa mara moja 2014 chini ya kocha Joseph Omog.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Dk. Mkwizu: Afrika tudumishe utamaduni

Spread the love  MWENYEKITI wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Mkoa wa...

Michezo

‘EONII’ kuteka tasnia ya filamu

Spread the love  UZINDUZI wa Filamu ya Kisayansi ya ‘EONII’ uliofanyika Mei...

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

error: Content is protected !!