Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Tangulizi Hakimu amgomea wakili wa Mbowe
Tangulizi

Hakimu amgomea wakili wa Mbowe

Viongozi wa Chadema wakiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

THOMAS Simba, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam amegomea ombo la wakili wa Freeman Mbowe na wenzake, la kuomba siku 21 za maandalizi ya ushahidi. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa na wenzake wanane, wanakabiliwa na tuhuma za kufanya uchochezi kwenye shitaka namba 221/2018 katika mahakama hiyo.

Wakili Kibatala aliiomba mahakama hiyo siku 21 kwa ajili ya kufanya maandilizi ya kupeleka utetezi, hata hivyo leo tarehe 21 Oktoba 2019, Hakimu Simba alisema ‘haiwezekani’ upande wa utetezi kupewa siku 21 na badala yake amewapa siku 14.

Mbali na kutoa siku 14 Hakimu Simba amesema, ombi lingine la Wakili Kibatala la kuomba kielelezo namba P4 ambacho ni (Min Div) – mbili zilizotolewa mahakamani hapo na shahidi wa saba wa serikali Koplo Charles, haliwezekani.

Hakimu Simba amesema, kielelezo hiko hakiwezi kutolewa nje ya mahakama, isipokuwa kitolewa kwa ajili ya kuoneshwa chini ya utawala wa mahakama kwenye ukumbi wa mahakamani na usimamizi wa mahakama kama ilivyokuwa kwa upande wa Jamhuri.

Viongozi tisa wa Chadema akiwemo Freeman Mbowe, mwenyekiti wa chama hicho Taifa, wanakabiliwa na kesi ya uchochezi namba 221/2018 kwenye mahakama hiyo ambayo iliwakuta na na kesi ya kujibu.

Pia yumo Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu-Taifa; John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu – Bara na Salumu Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu -Z’Bar.

Wengine ni Ester Matiko Mbunge wa Tarime Mjini; Halima Mdee, Mbunge wa Kawe; Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini; John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini na Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini.

Hakimu Simba wakati anatoa uamuzi huo, upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Faraja Nchimbi Wakili wa Serikali Mkuu, Wankyo Simon Wakili wa Serikali Mwandamizi, Salim Msemo Wakili wa Serikali na Jacklin Nyantori Wakili wa Serikali huku upande wa Utete ukiwakilishwa na Wakili Jeremiah Mtobesya na Hekima Mwasipu.

Baada ya kutoa uamuzi huo, Hakimu Simba ameahirisha shauri hilo na kusema, litasikilizwa tarehe 4, 5 na 8 Novemba 2019.

Viongozi hao kwa makosa 13  yakiwamo kufanya maandamano kinyume cha sheria, kutoa maneno ya uchochezi na kufanya kusanyiko lisilohalali lililosababisha mauaji ya Mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwelina Akwelin.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!