Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Umeme kukatika Dar es Salaam
Habari Mchanganyiko

Umeme kukatika Dar es Salaam

Mafundi umeme wakiwa kazini
Spread the love

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO), limetangaza katizo la umeme katika baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Ilala na Temeke, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa tangazo hilo, katizo hilo litatokea kesho tarehe 22 Oktoba 2019, kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi 10:30 jioni, kwenye njia ya Msongo wa 132KV ili kuruhusu kazi ya kuungwa kebo ya Transfoma mpya.

Tangazo hilo limeeleza kuwa, Transfoma hiyo mpya ina uwezo mkubwa wa Megawati 300MVA, ambayo itasaidia kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme kwa Jiji la Dar es Salaam, Zanzibar na Pwani.

Maeneo yatakayokumbwa na katizo hilo ni pamoja na, Buguruni, Vingunguti, Tazara, Gongo la Mboto, Ukonga, Mombasa, Mzambarauni, Pugu.

Maeneo mengine ni Yombo, Kitunda, Machimbo, Mwanagati, Mbondole pamoja na baadhi ya maeneo ya Tabata.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!