Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Taasisi za dini kufanyiwa uhakiki
Habari Mchanganyiko

Taasisi za dini kufanyiwa uhakiki

Spread the love

OFISI ya Msajili wa Jumuiya za Kijamii na Taasisi za Kidini, kufanya uhakiki wa taasisi na jumuiya hizo, zilizopo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Kwa mujibu wa barua iliyotolewa tarehe 30 Septemba 2019 na Meja Jenerali, Jacob Kingu, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, zoezi hilo la uhakiki litaanza Oktoba 7 hadi 18 mwaka huu.

“Awamu ya nne ya zoezi la uhakiki itafanyika katika mikoa ya Mwanza, Geita, Mara, Simiyu, Kagera na Shinyanga. Zoezi litafanyika kwenye Kituo cha Uhakiki kilichopo katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi jioni,” inaeleza barua hiyo.

Barua hiyo imeeleza kuwa, wakati wa uhakiki, taasisi na jumuiya husika zinatakiwa kuwa na nyaraka mbalimbali ikiwemo cheti halisi na kivuli cha usajili, stakabadhi ya mwisho ya malipo ya ada iliyolipwa hivi karibuni, katika iliyopitishwa na msajili. Taarifa ya Mkutano mkuu wa mwaka pamoja na taarifa ya fedha ya mwaka.

Barua hiyo imeeleza kuwa, taasisi zitakazoshindwa kuhakikiwa kwa muda uliopangwa zitaondolewa kwenye daftari la msajili.

“Aidha, taasisi za sini na jumuiya za kijamii ambazo hazijasajiliwa zinatakiwa kufika wakati wa zoezi la uhakiki kwa ajili ya kupewa utaratibu wa kupata usajili,” inaeleza barua hiyo.

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

error: Content is protected !!