SERIKALI imewataka viongozi wa vyama vya watu wenye ulemavu kuwa wabunifu katika kuibua miradi, badala ya kutegemea wafadhili. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Hayo yalielezwa leo tarehe 12 Septemba 2019 bungeni na Naibu Waziri,Ofisi ya Waziri Mkuu, Stella Ikupa akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum, Amina Mollel (CCM).
Katika swali la nyongeza Molele alitaka kujua, serikali imejipangaje kupipatia ruzuku vyama vya watu ulemavu ili viweze kujiendesha badala ya kutumia muda mwingi kutegemea misaada.
Awali katika swali la msingi la mbunge wa Bumbwini, Muhammed Amour Muhammed (CUF), alitaka kujua serikali imejipanga vipi katika kuzisaidia na kuziwezesha tasisi zinazoshughulikia watu wenye ulemavu.
Akijibu swali hilo Ikupa amesema, pamoja na serikali kuwezesha vyama vya watu wenye ulemavu lakini umefika wakati ambao viongozi wa vyama hivyo kuwa wabunifu.
Amesema, iwapo viongozi wa vyama hivyo wakiwa wabunifu, itasaidia kwa kiasi kikubwa kuweza kujitegemea na kuondokana na utegemezi ambao unaweza kujitokea na watakuwa wameepukana na kusubiri misaada.
Aidha, amesema kwa mujibu wa sera ya taifa ya maendeleo na huduma kwa watu wenye ulemavu ya mwaka 2004 na sharia na 9 ya mwaka 2010 ya watu wenye ulemavu, serikali inayo majukumu mbalimbali ya kuhakikisha taasisi zinazowahudumia watu wenye ulemavu zinatoa huduma stahiki.
Leave a comment