Friday , 3 May 2024
Habari za Siasa

Nape aungama kwa JPM

Spread the love

NAPE Nnauye, Mbunge wa Mtama, leo tarehe 10 Agosti 2019 amekwenda kuungama kwa Dk. John Magufuli, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Mbunge huyo kijana, amechukua hatua hiyo siku sita baada ya January Makamba (Bumbuli) na Willium Njeleja (Sengerema) kwenda kumwomba radhi kwa kile kilichoelezwa na Rais Magufuli ‘kumtukana’.

Nape amekwenda kumtembelea Rais Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam na kumwomba radhi kutokana na kuvuja kwa sauti za mazungumzo kati yake na Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje Mstaafu dhidi ya Rais Magufuli.

Mwanasia huyo ambaye aliwahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM amesema, ameamuo kuomba radhi Rais Magufuli ili kulinda husiano wao na kueleza, anamheshimu kama baba yake na kiongizi wa nchi na chama chake.

“Kwanza nimekuja kumuona baba yangu lakini ni mwenykiti wa chama changu na rais wangu. Sababu wote wanajua mambo yaliyopita, yametokea mengi katikati na mimi kama mtoto wa CCM mwanaye nimekosea, ni vizuri niongee na baba yangu.

“…ameniambia amenisamehe, amenishauri namshukuru sana kwa kunisamehe na lakini pili kunielekeza namna ya kufanya ninakokwenda.”

Rais Magufuli amesema, amemsamehe ingawa ilikua mgumu kuchukua hatua hiyo akisema, Nape alimsumbua akimtaka amsamehe ikiwemo kwa kumtumia ujumbe mfupi wa simu usiku wa manane pia kupitia Mama Maria Nyerere.

“Na mimi nimemsamehe kwa dhati, sisi tumeumbwa kusamehe ingawa kusamehe kunaumiza, lakini nimemsamehe,” amesema Rais Magufuli.

Tazama video kamili hapo chini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

error: Content is protected !!