Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Ujerumani yaipa Tanzania Bil 32
Habari Mchanganyiko

Ujerumani yaipa Tanzania Bil 32

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imepatiwa msaada wa Sh. 32.74 bilioni kutoka Ujerumani kwa ajili ya kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi, pamoja na kudhibiti maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (V.V.U) kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Fedha hizo zimetolewa na Ujerumani kwa ajili ya utekelezaji wa awamu ya tatu ya mradi wa ‘Tumaini la Mama’ unaotoa huduma kwa kina mama na watoto wanaotoka kwenye kaya masikini, unaotekelezwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Mkataba wa msaada huo ulisainiwa jana tarehe 9 Septemba 2019 jijini Dar es Salaam na Doto James , Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Dk. Annika Calov, Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo, James amesema sehemu ya fedha hizo zitatumika kununua vifaa tiba vinavyohusiana na afya ya uzazi kwa ajili ya kuimarisha utoaji wa huduma za afya katika mikoa iliyochaguliwa kunufaika na mradi huo.

 Dk. Calov amesema fedha hizo zitasaidia kuboresha afya ya mama na mtoto pamoja na kuzia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda na mtoto katika mikoa ya Mbeya, Songwe, Tanga, Lindi na Mtwara.

Kwa upande wake Bernard Konga, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF amesema tangu mradi huo uanze mwaka 2012, kina mama 1,157,191 wamenufaika nao kwa kuwa na bima ya afya kupitia shirika hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yatoa msaada wa mil. 20 kwa waathirika mafuriko Hanang

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) sambamba na wafanyakazi wa...

Habari Mchanganyiko

Polisi wadaka mirungi kwenye basi la Extra Luxury

Spread the loveJeshi la polisi mkoani Kilimanjaro limekamata shehena ya dawa za...

Habari Mchanganyiko

Oryx yaungana na jamii kuwafariji waathirika maporomoko Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeungana na Watanzania kutoa pole...

Habari Mchanganyiko

Amsons Group watoa milioni 100 waathirika maafa Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...

error: Content is protected !!