Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ujerumani yaipa Tanzania Bil 32
Habari Mchanganyiko

Ujerumani yaipa Tanzania Bil 32

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imepatiwa msaada wa Sh. 32.74 bilioni kutoka Ujerumani kwa ajili ya kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi, pamoja na kudhibiti maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (V.V.U) kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Fedha hizo zimetolewa na Ujerumani kwa ajili ya utekelezaji wa awamu ya tatu ya mradi wa ‘Tumaini la Mama’ unaotoa huduma kwa kina mama na watoto wanaotoka kwenye kaya masikini, unaotekelezwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Mkataba wa msaada huo ulisainiwa jana tarehe 9 Septemba 2019 jijini Dar es Salaam na Doto James , Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Dk. Annika Calov, Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo, James amesema sehemu ya fedha hizo zitatumika kununua vifaa tiba vinavyohusiana na afya ya uzazi kwa ajili ya kuimarisha utoaji wa huduma za afya katika mikoa iliyochaguliwa kunufaika na mradi huo.

 Dk. Calov amesema fedha hizo zitasaidia kuboresha afya ya mama na mtoto pamoja na kuzia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda na mtoto katika mikoa ya Mbeya, Songwe, Tanga, Lindi na Mtwara.

Kwa upande wake Bernard Konga, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF amesema tangu mradi huo uanze mwaka 2012, kina mama 1,157,191 wamenufaika nao kwa kuwa na bima ya afya kupitia shirika hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!