Monday , 11 December 2023
Habari za Siasa

Nape aungama kwa JPM

Spread the love

NAPE Nnauye, Mbunge wa Mtama, leo tarehe 10 Agosti 2019 amekwenda kuungama kwa Dk. John Magufuli, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Mbunge huyo kijana, amechukua hatua hiyo siku sita baada ya January Makamba (Bumbuli) na Willium Njeleja (Sengerema) kwenda kumwomba radhi kwa kile kilichoelezwa na Rais Magufuli ‘kumtukana’.

Nape amekwenda kumtembelea Rais Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam na kumwomba radhi kutokana na kuvuja kwa sauti za mazungumzo kati yake na Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje Mstaafu dhidi ya Rais Magufuli.

Mwanasia huyo ambaye aliwahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM amesema, ameamuo kuomba radhi Rais Magufuli ili kulinda husiano wao na kueleza, anamheshimu kama baba yake na kiongizi wa nchi na chama chake.

“Kwanza nimekuja kumuona baba yangu lakini ni mwenykiti wa chama changu na rais wangu. Sababu wote wanajua mambo yaliyopita, yametokea mengi katikati na mimi kama mtoto wa CCM mwanaye nimekosea, ni vizuri niongee na baba yangu.

“…ameniambia amenisamehe, amenishauri namshukuru sana kwa kunisamehe na lakini pili kunielekeza namna ya kufanya ninakokwenda.”

Rais Magufuli amesema, amemsamehe ingawa ilikua mgumu kuchukua hatua hiyo akisema, Nape alimsumbua akimtaka amsamehe ikiwemo kwa kumtumia ujumbe mfupi wa simu usiku wa manane pia kupitia Mama Maria Nyerere.

“Na mimi nimemsamehe kwa dhati, sisi tumeumbwa kusamehe ingawa kusamehe kunaumiza, lakini nimemsamehe,” amesema Rais Magufuli.

Tazama video kamili hapo chini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Jaji Kiongozi akerwa wananchi kukosa imani na mahakama

Spread the loveWATENDAJI wa Mahakama ya Tanzania, wametakiwa kuweka mikakati itakayosaidia kurejesha...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

error: Content is protected !!