Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Tangulizi IGP Sirro: Sasa washughulikieni wauaji
Tangulizi

IGP Sirro: Sasa washughulikieni wauaji

IGP Simon Sirro
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro ameagiza polisi nchini kuwachukulia hatua watu wanaoua wenzao kwa kuwatuhumu ushirikina. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

IGP Sirro ametoa agizo wakati akizungumza na maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani Tabora leo tarehe 31 Agosti 2019, amelitaka jeshi hilo kuwafikisha mahakamani watu wanaotuhumiwa kufanya mauaji hayo.

“Bahati nzuri mlishaunda kikosi cha kupambana na haya mauaji yanayotokana na imani za kishirikina, kwa hiyo kitafanya kazi kubwa kuhakikisha hawa watu wanaohusika wanakamatwa, na si kukamatwa peke yake bali kuhakikisha kwamba wapelekwe mahakamani,” ameagiza IGP Sirro.

Aidha, IGP Sirro amewataka viongozi wa dini wa kisiasa kutoa elimu kwa jamii kuhusu suala hilo, ili waache mara moja.

“Kwenye hili suala la mauaji viongozi wa dini watusaidie sababu kukiwepo na hofu ya Mungu haya mauji yatapungua. Yamepungua lakini bado yapo,” amesema IGP Sirro.

Wakati huo huo, IGP Sirro ameagiza Jeshi la Polisi kufanya doria usiku na mchana ili kukomesha matukio ya wizi.

“Lakini matukio mengine yanayojitokeza ni uvunjaji mdogopmdogo ambao nimeelekeza doria zifanyike zaidi za usiku na mchana,” ameagiza IGP Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!