Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Tangulizi IGP Sirro: Sasa washughulikieni wauaji
Tangulizi

IGP Sirro: Sasa washughulikieni wauaji

IGP Simon Sirro
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro ameagiza polisi nchini kuwachukulia hatua watu wanaoua wenzao kwa kuwatuhumu ushirikina. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

IGP Sirro ametoa agizo wakati akizungumza na maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani Tabora leo tarehe 31 Agosti 2019, amelitaka jeshi hilo kuwafikisha mahakamani watu wanaotuhumiwa kufanya mauaji hayo.

“Bahati nzuri mlishaunda kikosi cha kupambana na haya mauaji yanayotokana na imani za kishirikina, kwa hiyo kitafanya kazi kubwa kuhakikisha hawa watu wanaohusika wanakamatwa, na si kukamatwa peke yake bali kuhakikisha kwamba wapelekwe mahakamani,” ameagiza IGP Sirro.

Aidha, IGP Sirro amewataka viongozi wa dini wa kisiasa kutoa elimu kwa jamii kuhusu suala hilo, ili waache mara moja.

“Kwenye hili suala la mauaji viongozi wa dini watusaidie sababu kukiwepo na hofu ya Mungu haya mauji yatapungua. Yamepungua lakini bado yapo,” amesema IGP Sirro.

Wakati huo huo, IGP Sirro ameagiza Jeshi la Polisi kufanya doria usiku na mchana ili kukomesha matukio ya wizi.

“Lakini matukio mengine yanayojitokeza ni uvunjaji mdogopmdogo ambao nimeelekeza doria zifanyike zaidi za usiku na mchana,” ameagiza IGP Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme wang’oa vigogo TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewahamisha waliokuwa vigogo wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mgogoro wa ardhi Kiteto: Wakulima wadaiwa kutwanga risasi ng’ombe wa wafugaji Kiteto

Spread the loveMGOGORO kati ya wafugaji na wakulima katika Kijiji cha Lembapuli,...

Habari za SiasaTangulizi

Mchengerwa amtumbua mkurugenzi Busega

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na...

error: Content is protected !!