Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Mkuu aongoza watanzania mazishi ya watu waliofariki ajali ya moto
Habari Mchanganyiko

Waziri Mkuu aongoza watanzania mazishi ya watu waliofariki ajali ya moto

Spread the love

KASSIM Majaliwa Waziri Mkuu Tanzania ameongoza maelfu ya watanzania mazishi ya watu zaidi ya 60 waliofariki kwenye mlipuko wa  lori la mafuta  baada ya kupinduka jana mtaa wa Itigi Msamvu mkoani Morogoro, Anaripoti Hamisi Mguta, Dodoma … (endelea).

Leo tarehe 11 Waziri Mkuu amefika Morogoro kwa ajili ya kuungana na wafiwa pamoja na watanzania kwenye kuaga miili ya watu waliofariki kwenye ajali hiyo ambapo watazikwa eneo la Kola.

“Tunatamani hawa ndugu zetu kuwazika kwenye kando ya barabara (Msamvu)  na kuweka mnara katika eneo hilo lakini ufinyu wa eneo hilo hatuna budi kwenda kuwazika eneo la Kola” amesema Majaliwa

Wakati huo huo ameeleza namna Rais John Magufuli alivyowapokea majeruhi wa tukio hilo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na kuwapa pole .

Amesema kuwa Rais Magufuli ameongea na majeruhi mmoja mmoja kwa wale wenye kuweza kuzungumza na pia ameridhishwa  na mna Muhimbili wanavyotoa huuduma kwa majeruhi.

Ameeleza kuwa waliofariki hadi sasa wamefikia idadi ya watu 72  na  majeruhi wapo 59 , waliokuwepo Hospitali ya Rufaa ya Morogoro  majeruhi 16 kule Muhimbili wapo 43.

Amewashukuru wananchi na majeshi mbalimbali likiwemo jeshi la Wananchi JWTZ, Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto, na majeshi mengine nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!