Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Mkuu aongoza watanzania mazishi ya watu waliofariki ajali ya moto
Habari Mchanganyiko

Waziri Mkuu aongoza watanzania mazishi ya watu waliofariki ajali ya moto

Spread the love

KASSIM Majaliwa Waziri Mkuu Tanzania ameongoza maelfu ya watanzania mazishi ya watu zaidi ya 60 waliofariki kwenye mlipuko wa  lori la mafuta  baada ya kupinduka jana mtaa wa Itigi Msamvu mkoani Morogoro, Anaripoti Hamisi Mguta, Dodoma … (endelea).

Leo tarehe 11 Waziri Mkuu amefika Morogoro kwa ajili ya kuungana na wafiwa pamoja na watanzania kwenye kuaga miili ya watu waliofariki kwenye ajali hiyo ambapo watazikwa eneo la Kola.

“Tunatamani hawa ndugu zetu kuwazika kwenye kando ya barabara (Msamvu)  na kuweka mnara katika eneo hilo lakini ufinyu wa eneo hilo hatuna budi kwenda kuwazika eneo la Kola” amesema Majaliwa

Wakati huo huo ameeleza namna Rais John Magufuli alivyowapokea majeruhi wa tukio hilo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na kuwapa pole .

Amesema kuwa Rais Magufuli ameongea na majeruhi mmoja mmoja kwa wale wenye kuweza kuzungumza na pia ameridhishwa  na mna Muhimbili wanavyotoa huuduma kwa majeruhi.

Ameeleza kuwa waliofariki hadi sasa wamefikia idadi ya watu 72  na  majeruhi wapo 59 , waliokuwepo Hospitali ya Rufaa ya Morogoro  majeruhi 16 kule Muhimbili wapo 43.

Amewashukuru wananchi na majeshi mbalimbali likiwemo jeshi la Wananchi JWTZ, Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto, na majeshi mengine nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!