Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli ataja sababu kumteua Bashe
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli ataja sababu kumteua Bashe

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ametaja sababu za kumteua Hussein Bashe, Mbunge wa Nzega kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Kilimo. Anaandika Regina Mkonde…(endelea).

Akizunguza baada ya kuwaapisha Bashe na George Simbachawene, Rais magufuli leo tarehe 22 Julai 2019, amesema amekuwa akimsikiliza Bashe anapochambua masuala ya kilimo bungeni.

Kutokana na hali hiyo, ameamua kumteua kwenye nafasi hiyo ili yale aliyokuwa akiyazungumza bungeni kuhusu kilimo, akayafanyie kazi.

“Nimekuwa nikikusikiliza vizuri bungeni, umetoa uchambuzi kuhusu kilimo nimeupenda, sasa zile zilikuwa bungeni nataka sasa ukaziweke kwenye practical (vitendo).

“…ni matumaini yangu kwamba yale ambayo uliyafikiria, umeyashauri, ukayatekeleze na mimi ni matumaini sababu sekta ya kilimo ni muhimu,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesema, kuna wizi mkubwa kwenye sekta ya kilimo na kwamba anafahamu changamoto inayopata bodi ya sukari.

“Bodi ya sukari inapitia changamoto nyingi sana, inapigwa vita na wafanyabaishara wa sukari, tukasema hapana, haiwezi tunakuwa tunaletewa masukari ya hovyo, yameexpire (yameisha muda wake), yanaletwa kwenye nchi yetu.

“Ni matumaini yangu hayo mkayajoin (mkayaunganishe) vizuri, changamoto zipo, mkisimama kwa umoja wenu mtayamaliza. Kule Kagera tumewaambia wauze kahawa wawekezaji wa nje waje lakini lazima wanunue 1500 na kuendelea kwa kilo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

error: Content is protected !!