Friday , 2 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli ataja sababu kumteua Bashe
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli ataja sababu kumteua Bashe

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ametaja sababu za kumteua Hussein Bashe, Mbunge wa Nzega kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Kilimo. Anaandika Regina Mkonde…(endelea).

Akizunguza baada ya kuwaapisha Bashe na George Simbachawene, Rais magufuli leo tarehe 22 Julai 2019, amesema amekuwa akimsikiliza Bashe anapochambua masuala ya kilimo bungeni.

Kutokana na hali hiyo, ameamua kumteua kwenye nafasi hiyo ili yale aliyokuwa akiyazungumza bungeni kuhusu kilimo, akayafanyie kazi.

“Nimekuwa nikikusikiliza vizuri bungeni, umetoa uchambuzi kuhusu kilimo nimeupenda, sasa zile zilikuwa bungeni nataka sasa ukaziweke kwenye practical (vitendo).

“…ni matumaini yangu kwamba yale ambayo uliyafikiria, umeyashauri, ukayatekeleze na mimi ni matumaini sababu sekta ya kilimo ni muhimu,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesema, kuna wizi mkubwa kwenye sekta ya kilimo na kwamba anafahamu changamoto inayopata bodi ya sukari.

“Bodi ya sukari inapitia changamoto nyingi sana, inapigwa vita na wafanyabaishara wa sukari, tukasema hapana, haiwezi tunakuwa tunaletewa masukari ya hovyo, yameexpire (yameisha muda wake), yanaletwa kwenye nchi yetu.

“Ni matumaini yangu hayo mkayajoin (mkayaunganishe) vizuri, changamoto zipo, mkisimama kwa umoja wenu mtayamaliza. Kule Kagera tumewaambia wauze kahawa wawekezaji wa nje waje lakini lazima wanunue 1500 na kuendelea kwa kilo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

Habari Mchanganyiko

Dk. Gwajima atoa maelekezo kwa maofisa maendeleo nchini

Spread the love  WAZIRI wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto,...

error: Content is protected !!