Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliouwa Watanzania Msumbiji wanaswa, mmoja afariki
Habari Mchanganyiko

Waliouwa Watanzania Msumbiji wanaswa, mmoja afariki

IGP Simon Sirro
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro amesema, watu watano wanaoshukiwa kuhusika katika tukio la mauaji ya Watanzania tisa nchini Msumbiji, wanashikiliwa na vyombo vya dola nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

IGP Sirro amesema hayo katika hafla ya uzinduzi wa nyumba 20 za polisi mkoani Geita leo tarehe 15 Julai 2019.

Aidha, IGP Sirro amesema mtuhumiwa mmoja kati ya watano waliokamatwa, amefariki dunia.

“Hata tukio la Msumbiji, niliahidi kwa Watanzania kwamba waliofanya hilo tukio, damu ya Watanzania haipotei bure. Mpaka sasa watu watano wamekamatwa na mmoja wao ametangulia mbele ya haki na wanatajana,” amesema IGP Sirro.

Wakati huo huo, IGP Sirro amesema mpango wa utekelezaji wa tukio hilo ulifanyika nchini Tanzania, huku utekelezaji wake ukifanyika nchini Msumbiji.

IGP Sirro amesema, Jeshi la Polisi nchini linashirikiana na Jeshi la Polisi la Msumbiji kuwachukulia hatua waliohusika na mauaji hayo.

“Inaonekana kwa kweli plan ‘mpango’ yote ilifanyika nchini kwetu, tukio lilifanyika Msumbiji. Kimsingi wote wamepatikana wanaendelea kutajana, operesheni inafanyika kwa kushirikiana na wenzetu wa Msumbiji,” amesema IGP Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!