Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Kabudi: Wameninukuu vibaya, sijasema Azory amefariki
Habari MchanganyikoTangulizi

Prof. Kabudi: Wameninukuu vibaya, sijasema Azory amefariki

Spread the love

PROFESA Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, amekanusha kauli inayosambaa katika mitandao ya kijamii ya kwamba amethibitisha kuwa mwanahabari Azory Gwanda amefariki dunia. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Dk. Hassan Abass, Msemaji Mkuu wa Serikali katika ukurasa wake wa Twitter, imemnukuu Prof. Kabudi akisema kwamba, mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Azory yuko hai au amefariki.

Prof. Kabudi amesema amepokea kwa masikitiko tafsiri zilizotolewa na baadhi ya watu, kufuatia kauli yake aliyoitoa wakati akihojiwa kwenye kipindi cha BBC Focus on Africa, kwa kuwa tafsiri hizo zimemnukuu kimakosa.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa potofu zinazoendelea kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii ikinukuu kimakosa mahojiano yangu kwenye kipindi cha BBC FOCUS ON AFRICA zikidai kuwa nimethibitisha kwamba mwanahabari Azory Gwanda amefariki dunia,” amefafanua Prof. Kabudi na kuongeza.

“Mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Azory yuko hai au amefariki. Vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuchunguza tukio hilo na matukio mengine yaliyotokea katika machafuko ya Kibiti, Pwani yaliyosababisha ama watu kadhaa kupoteza maisha au kupotea.”

Prof. Kabudi amesema katika mahojiano hayo alieleza kwamba tukio hilo lililotokea Kibiti mkoani Pwani ni la kuhuzunisha na wapo Watanzania waliouwawa na wengine kupotea.

“Hii sio tafsiri sahihi kuhusu kile nilichokisema. Katika mahojiano hayo nilieleza kuwa tukio lililotokea Kibiti lilikuwa ni la kuhuzunisha na wapo watanzania waliouwawa na wengine kupotea. Sikuthibitisha kuwa Azory Gwanda amefariki.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!