Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polepole: Watu mashuhuri wanaokufa ni wa CCM
Habari Mchanganyiko

Polepole: Watu mashuhuri wanaokufa ni wa CCM

Spread the love

HUMPHREY Polepole, Katibu wa Itikati na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema, watu wengi mashuhuri wanaokufa huwa wanachama wa chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akitoa salamu za pole kwenye kwenye shughuli ya kuuaga mwili wa Dk. Reginald Abraham Mengi iliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam leo tarehe 7 Mei 2019, Polepole amesema CCM ina bahati ya kuwa na watu maarufu.

“Kwenye chama chetu tuna bahati, watu wote mashuhuri wanaokufa ni wana CCM, Mzee Menegi wala hakujificha, alikuwa rafiki wa Rais Magufuli (Rais John Magufuli,” amesema.

Kwenye salamu zake kwa wafiwa, Polepole amewataka kutokata tamaa na kuwa imara kama alivyokuwa Dk. Mengi.

“Tusikate tamaa, tupambane kama mtu, taasisi na taifa. Dk. Mengi ametufundisha kutafuta. Alikuwa mtu madhubuti, makini na ambaye ametuonesha kwamba, inawezekana,” amesema.

Amesema, baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ndani ya chama hicho hakukuwa sawa kidogo na kwamba, ushauri wake umesaidia kuweka mambo sawa.

Ameeleza kuwa, ni vizuri Watanzania wakaendeleza dhamira ambayo Dk. Mengi aliyoonesha kama mfano huku akisisitiza kuendelea kuwekwa vizuri mazingira ya sekta binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!