Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Michezo Pondamali afunguka safari ya Lagos 1980
Michezo

Pondamali afunguka safari ya Lagos 1980

Spread the love

MLINDA mlango wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania, Juma Pondamali amesema kuwa safari ya timu hiyo kufuzu katika michuano ya lililokuwa kombe la mataifa huru ya Afrika mwaka 1980 haikuwa rahisi kwa kuwa walikutana na timu nyingi ngumu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)

Akizungumza katika mahojiano maalumu na MwanaHALISI TV, Pondamali amesema kuwa kundi waliopangiwa kwa ajili ya kusaka tiketi ya michuano hiyo lilikuwa na timu tano na ilihitajika kupita moja tu.

“Kipindi kile kulikuwa na timu kama Kenya (Harambee Star), Madagasca, Zambia, Tanzania na Mouritius , kundi lilikuwa na timu tano lakini hapo ilikuwa inapita timu moja, sasa kama ilikuwa hivyo basi makundi yetu yalikuwa magumu kuliko haya,” alisema Pondamali.

Golikipa huyo aliongezea kuwa hata walipoenda kwenye michuano hiyo Lagos walipangiwa kundi gumu kiasi cha kuhisi kama walionewa kwa kuwa kundi hilo lilikuwa na miamba ya soka wa Afrika kwa wakati huyo.

“Tunaweza kusema CAF walituonea maana huo mziki waliotuwekea ulikuwa hatari, kwa sababu tulipangiwa kundi moja na mwenyeji ambaye ni Nigeria, Misri na Ivory Coast. Tulihisi kama walituonea,” aliongezea Pondamali.

Pondamali ambaye kwa sasa ni kocha wa makipa wa klabu ya Yanga ambayo inashiriki Ligi Kuu Tanzania Bara na kuna muda alishawahi kuwa kocha wa makipa wa Taifa Stars.

Tazama mahojiano kamili hapo chini

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!