Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo JPM: Sikutaka fedheha, atoa zawadi ya karne kwa Taifa Stars
Michezo

JPM: Sikutaka fedheha, atoa zawadi ya karne kwa Taifa Stars

Spread the love

RAIS John Magufuli amekutana na Timu ya Soka ya Taifa-Taifa Stars- leo tarehe 25 Machi 2019 ambapo amewaeleza, alishindwa kwenda uwanjani kuangalia mechi kwa kuogopa fedheha. Anaripoti Bupe Mwakiteleko…(endelea).

“Niliogopa fedheha, niliamua kubaki hapa hapa nyumbani kuangualia mpira,” amewaambia wachezaji hao Ikulu jijini Dar es Salaam.

Wachezaji wa Taifa Stars walioambatana na viongozi mbalimbali wa nchi, Shirikisho la Soka nchini (TFF) na wachezaji wa zamani waliosakilishwa na Peter Tino walialikwa na Rais Magufuli kwenye Ikula kula chakula cha mchana leo.

Akizungumzia mechi ya jana tarehe 24 Machi 2019 Rais Magufuli ameeleza kufurahishwa na kiwango cha wachezaji wa Taifa Stars kwa kuonesha kiwango kikubwa.

Kwenye mchezo huo dhidi dhidi ya Uganda, Tanzania ilishinda 3-0 na hatimaye kufuzu michuano ya AFCON inayotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu nchini Misri.

“.. Nimeamini kuwa, kumbe tunaweza lakini niliona baada ya kufunga moja na kutokana na Tanzania hii wanavyocheza, nikaamini goli litarudi sasa hivi. Mke wangu akaniambia Tanzania leo tutashinda, nikamwambia wewe unajua nini?” amesema Rais Magufuli na kuongeza:

“Nilipoangalia kwenye televisheni zetu nikaona wachezaji wanasifiwa sifiwa nikaamua kubadilisha na kuweka Super Sport na huko nikaona wanawasifia, nikaona kweli wanacheza vizuri.”

Rais Magufuli amesema, baada ya Stars kushinda goli la tatu, alihamia kuangalia mechi ya Cape Vade na Lesotho kuangalia kama timu hiyo (Lesotho) imefungwa “kule nikaona bila bila.”

Katika ghafla hiyo ya chakula cha mchana na wachezaji pia uongozi wa TFF Rais Magufuli amesema, jana tarehe 24 Stars walimaliza machungu yake.

Kutokana na furaha hiyo, Rais Magufuli amemwagiza Kasim Majaliwa, Waziri Mkuu kuhakikisha wachezaji hao wanapatiwa viwanja jijini Dodoma.

“Mimi nimeona niwape zawadi kidogo, sina kitu lakini kwa niaba ya Watanzania nimeamua kuwapa zawadi. Nimeamua kuwapa kila mmoja viwanja Dodoma. Tena itakuwa vizuri viwanja hivyo viwaka wapamoja,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesisitiza kuwa, kama Taifa Stars itaendelea kucheza vizuri kama ilivyocheza na Uganda, inaweza kufika robo ama nusu fainali.

Amesisitiza kuwa, wachezaji hao kama wataendelea kucheza vizuri, wataonekana na watachukuliwa kwenda kucheza nje (mkiendelea kucheza hivyo wengi watachukuliwa. Hilo ndio ombi langu kwa kuwa mchezo ni biashara na biashara hii tusiilazie damu.”

Amesema, Wizara ya Michezo sasa anaweza kuzungumza nao vizuri . “Nataka waziri akiniambia tunashinda, tushinde kweli sio tushindwe. Nafuu anyamanze aseme bana hapa tunapigwa na haka katimu kadogo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!