Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Baada ya miezi minane mochwali, mwili kuzikwa wiki hii
Habari Mchanganyiko

Baada ya miezi minane mochwali, mwili kuzikwa wiki hii

Spread the love

FAMILIA ya marehemu Frank Kapange imeamua kuchukua mwili wa kijana wao uliohifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa zaidi ya miezi minane ili kufanya taratibu za mazishi wiki hii. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Familia hiyo iligoma kuchukua mwili wa Frank kwa ajili ya mazishi wakitaka uchunguzi ufanyike kuhusu chanzo cha kifo hicho kilichotokea tarehe 4 Juni 2018 ufanyike.

Familia ya Frank ilifungua shauri katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya wakiiomba mahakama kutoa amri ya kufanyiika kwa uchunguzi wa kifo cha kijana wao, lakini shauri hilo lilitupiliwa mbali. Kutokana na familia hiyo kutoridhika na uamuzi huo, walikata rufaa katika Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya ambayo pia iliifuta kesi hiyo baada ya kujiridhisha kwamba mlalamikaji hakufuata taratibu wakati wa kuifungua kesi hiyo.

Msemaji wa Familia ya Frank, Julius Kapange amesema wameuchukua mwili huo kwa ajili ya kufanya mazishi huku akiitupia lawama mahakama kwa kutotoa kibali cha kufanyika kwa uchunguzi wa kifo cha kijana wao.

“Kama familia imetusumbua sana siwezi kuendelea zaidi, ila nasikitika kwa sababu haki haijatendeka sababu lengo letu ilikuwa si kushindana na serikali, tulitegemea mahakama itatupa kibali cha kusema huyu marehemu amekufa kwa njia hii, angefanyiwa vipimo wakishapima watukabidhi mwili kwa amani tukazike, vipimo hatujapewa niliitwa tu nitambue maiti kama ni yangu nikatambua ni kijana wangu, “ amesema Kapange.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Dk. Godlove Mbwanji leo tarehe 26 Februari 2019  amesema  hospitali hiyo imesamehe gharama za kuhifadhia maiti katika kipindi hicho cha miezi nane na kwamba familia hiyo iko huru kufanya mazishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!