Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sugu aeleza aibu ya Uwanja wa Ndege Mbeya
Habari za Siasa

Sugu aeleza aibu ya Uwanja wa Ndege Mbeya

Uwanja wa Ndege wa Songwe
Spread the love

KIPINDI ambacho Uwanja wa Ndege wa Songwe, Mbeya unapogubikwa na ukungu, rubani hupata tabu kutua na wakati mwingine hulazimika hurudisha ndege Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ndege hushindwa kutua kutokana na kutokuwepo kwa taa hizo ambazo ni utaratibu wa kawaida kuwepo kwenye viwanja vyote. Kukosekana kwake husababisha kuvuruga ratiba za abiria pale wanaposhindwa kufika eneo husika kwa wakati kipindi cha ukungu.

Joseph Mbilinyi (Sugu), Mbunge wa Mbeya Mjini, ameihoji serikali lini itafanya marekebisho katika uwanja huo ili kuondoa na usumbufu unaowakabili wasafiri.

Akizungumza bungeni jijini Dodoma leo tarehe 4 Februari 2019, Sugu amesema, aliwahi kusafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya mara mbili bila ndege kutua kwenye uwanja huo na matokeo yake kurudishwa Dar es Salaam kutokana na wanjanja huo kutokua na taa za kusaidia marubani wakati wa ukungu.

“Lini ujenzi wa jengo la abiria utakamilika kwenye Uwanja wa Songwe, Mbeya? Sasa hivi kukiwa na ukungu na hakuna taa, rubani hatui.

“Mimi mwenyewe nimerudi Dar mara mbili kutokana na ndege kushindwa kutua sababu ya ukungu,” amesema Sugu.

Akijibu swali la Sugu, Mhandisi Isaack Kamwele, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi amesema, tayari serikali imetangaza tenda ya ujenzi wa uwanja huo hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!