Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Madiwani Chamwino watakiwa kuwakumbuka walemavu
Habari Mchanganyiko

Madiwani Chamwino watakiwa kuwakumbuka walemavu

Spread the love

MADIWANI wa Halmashauri ya Chamwino wametakiwa kuhakikisha majengo yanayojengwa yanakuwa na miundombinu rafiki kwa ajili ya watu wenye ulemavu. Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Ushauri huo umetolewa Katibu mkuu Taifa wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu, Jonas Lubago alipokuwa akizungumza na madiwani hao kwenye warsha ya utetezi wa watu wenye ulemavu wasioona (TLB) iliyofanyika wilayani Chamwino.

Lubago alisema madiwani kwa nafasi zao wanapaswa kuhakikisha wanasimamia majengo ya Umma kwenye kata na halmashauri na kata zao yanawekwa miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu ili na wao waweze kupatiwa huduma za msingi kama wanavopatiwa watu wengine.

“Kinachosikitisha ni kwa kuwa walio wengi madiwani wamekuwa wakitanguliza zaidi siasa zao kwenye masuala ya utekelezaji yanayohusu wanajamii badala ya kuwa wakweli kwenye nafasi zao,” alisema.

Akizungumza kwenye warsha hiyo iliyofadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la The Foundation Civil Association, alisema majengo mengi ya taasisi bado ni changamoto kubwa kwa jamii hiyo ya watu wenye ulemavu.

Wakizungumza kwenye kuchangia kwa nyakati tofauti madiwani hao walisema kuwa bado kuna changamoto kubwa ya watu wenye ulemavu katika kupata huduma zao za kimsingi kutokana na walio wengi kutothaminiwa na jamii.

Olipa Maganjila diwani viti maalum kata ya Chamwino, aliiomba halmashauri kutoa tamko kuwa majengo yote yanayotoa huduma za kijamii yakiwemo shule za msingi, sekondali na vituo vya afya yanakuwa rafiki kwenye miundombinu yake.

Diwani wa kata ya Buigiri Keneth Yindi, aliomba kuwepo na takwimu sahihi ya watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya vitongoji hadi wilaya ili waweze kuunda umoja utakaowasaidia kupata mikopo lwa ajili ya maendeleo yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wasioona wilaya ya Chamwino, Gabriel Masaka, alisema tatizo lililopo kwa madiwani wa halmashauri hiyo kwa watu wenye ulemavu ni kutoshirikishwa kwenye shughuli za kijamii.

Aidha changamoto nyingine pia ni ukosefu wa elimu kwa watu wanaoishi na walemavu hii ikiwa na pamoja na unyanyapaa uliopo wanaofanyiwa na familia wanazoishinazo.

Masaka alisema kuwa kutokana na baadhi ya changamoto hizo bado hata kwenye upande wa serikali itaendelea kuwasahau watu hao na kuwafanya kukosa haki zao za kimsingi ikiwemo elimu na afya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!