Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Ranieri kumrithi Jokanovic Fulham
Michezo

Ranieri kumrithi Jokanovic Fulham

Claudio Ranieri
Spread the love

MKUFUNZI wa zamani wa Leicester City, Claudio Ranieri ameteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa klabu ya Fulham inayoshiriki Ligi Kuu ya England mara baada ya kumtimua aliyekuwa kocha wao Slavisa Jokanovic, kutokana na matokeo mabovu ya timu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Ranieri amesema kuwa ni heshima kukubali mwaliko wa mmiliki wa klabu hiyo Shahid Khan na nafasi ya kuiongoza Fulham ambayo ni klabu kubwa kihistoria.

“Malengo makubwa ya Fulham hayapaswi kuishia katika ligi kuu nchini England,” alisema Ranieri.

Ikumbukwe Ranieri ndiyo kocha pekee aliyeiongoza Lecester City kutwaa taji lao la kwanza la Ligi Kuu England katika msimu wa mwaka 2016, akiwa na kikosi ambacho hakikughalimu kiasi kikubwa cha fedha kwenye usajiri.

Fulham ambayo kwa sasa inashika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi hiyo baada ya kupoteza michezo tisa kati ya 12 waliocheza na kuruhusu mabao 31, licha ya mmiliki wa klabu hiyo Shahid Khan kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwenye usajili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!