Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Korosho yaondoka na mawaziri wawili
Habari za SiasaTangulizi

Korosho yaondoka na mawaziri wawili

Spread the love

RAIS John Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya Baraza lake la Mawaziri ambapo Charles Mwijage na Dk. Charles Tizeba wametemwa. Anaandika Faki Sosi … (endelea).

Mwijage alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara huku Dk. Tizeba akiwa Waziri wa Kilimo.

Kwenye maadiliko hayo Mwita Waitara, Mbunge (mpya) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiteuliwa kuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI.

Mwita awali alikuwa Mbunge was Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam kupitia Chadema ambapo alijiuzulu na kurejea CCM kisha aliteuliwa kugombea ubunge kupitia chama hicho (CCM).

Taarifa iliyotumwa na Mkurugenzi ya mawasiliano ya Rais Ikulu Gerson Msigwa, imeeleza nafasi ya Dk. Tizeba imeshikwa na Japhet Hasunga, ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii.

Aidha katika nafasi ya viwanda na biashara iliyokuwa chini ya Mwijage, imechukuliwa na Joseph Kakunda, ambaye naye kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa TAMISEMI.

Pia Rais Magufuli amemteua Constantine John Kanyasu kuwa Naibu Waziri wa Maliasili na utalii, pamoja na kumteua Profesa Mary Mwanjelwa kuwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala bora.

Aidha Rais Magufuli, amemteua Innocent Lugha kuwa naibu Waziri wa Kilimo, na uteuzi wa viongozi unaanza Novemba 10.

Pamoja na hivyo Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mama Anna Abdallah wa uenyekiti wa Bodi ya Korosho, pia ameivunja Bodi ya Korosho.

Walioteuliwa wataapishwa Jumatatu Ikulu Jijini Dar es salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!