Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Korosho yaondoka na mawaziri wawili
Habari za SiasaTangulizi

Korosho yaondoka na mawaziri wawili

Spread the love

RAIS John Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya Baraza lake la Mawaziri ambapo Charles Mwijage na Dk. Charles Tizeba wametemwa. Anaandika Faki Sosi … (endelea).

Mwijage alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara huku Dk. Tizeba akiwa Waziri wa Kilimo.

Kwenye maadiliko hayo Mwita Waitara, Mbunge (mpya) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiteuliwa kuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI.

Mwita awali alikuwa Mbunge was Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam kupitia Chadema ambapo alijiuzulu na kurejea CCM kisha aliteuliwa kugombea ubunge kupitia chama hicho (CCM).

Taarifa iliyotumwa na Mkurugenzi ya mawasiliano ya Rais Ikulu Gerson Msigwa, imeeleza nafasi ya Dk. Tizeba imeshikwa na Japhet Hasunga, ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii.

Aidha katika nafasi ya viwanda na biashara iliyokuwa chini ya Mwijage, imechukuliwa na Joseph Kakunda, ambaye naye kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa TAMISEMI.

Pia Rais Magufuli amemteua Constantine John Kanyasu kuwa Naibu Waziri wa Maliasili na utalii, pamoja na kumteua Profesa Mary Mwanjelwa kuwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala bora.

Aidha Rais Magufuli, amemteua Innocent Lugha kuwa naibu Waziri wa Kilimo, na uteuzi wa viongozi unaanza Novemba 10.

Pamoja na hivyo Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mama Anna Abdallah wa uenyekiti wa Bodi ya Korosho, pia ameivunja Bodi ya Korosho.

Walioteuliwa wataapishwa Jumatatu Ikulu Jijini Dar es salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!