Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wampekua Zitto Kabwe nyumbani kwake
Habari za SiasaTangulizi

Polisi wampekua Zitto Kabwe nyumbani kwake

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini
Spread the love

IKIWA imepita siku moja tangu Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo , Zitto Kabwe kukamatwa na polisi jijini Dar es Salaam, leo Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni, limefanya upekuzi nyumbani kwake. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama cha ACT-Wazalendo na kuthibitishwa na Wakili wa Zitto, Jebra Kambole, inaeleza kuwa Mbunge huyo wa Kigoma Mjini aliwaongoza polisi hadi nyumbani kwake maeneo ya Masaki.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, baada ya polisi kukamilisha upekuzi, walimrudisha Zitto katika kituo cha Oysterbay na kwamba wakili wake anashughulikia suala la dhamana yake.

Kukamatwa kwa Zitto kumekuja siku kadhaa baada ya Jeshi la Polisi mkoani Kigoma kumtaka mwanasiasa huyo kujisalimisha polisi ili kuhojiwa kuhusu taarifa yake aliyoitoa Jumapili iliyopita, kuhusu mauaji ya askari na wananchi wa Kijiji cha Mpeta wilayani Uvinza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!