Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wampekua Zitto Kabwe nyumbani kwake
Habari za SiasaTangulizi

Polisi wampekua Zitto Kabwe nyumbani kwake

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini
Spread the love

IKIWA imepita siku moja tangu Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo , Zitto Kabwe kukamatwa na polisi jijini Dar es Salaam, leo Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni, limefanya upekuzi nyumbani kwake. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama cha ACT-Wazalendo na kuthibitishwa na Wakili wa Zitto, Jebra Kambole, inaeleza kuwa Mbunge huyo wa Kigoma Mjini aliwaongoza polisi hadi nyumbani kwake maeneo ya Masaki.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, baada ya polisi kukamilisha upekuzi, walimrudisha Zitto katika kituo cha Oysterbay na kwamba wakili wake anashughulikia suala la dhamana yake.

Kukamatwa kwa Zitto kumekuja siku kadhaa baada ya Jeshi la Polisi mkoani Kigoma kumtaka mwanasiasa huyo kujisalimisha polisi ili kuhojiwa kuhusu taarifa yake aliyoitoa Jumapili iliyopita, kuhusu mauaji ya askari na wananchi wa Kijiji cha Mpeta wilayani Uvinza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!