Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wampekua Zitto Kabwe nyumbani kwake
Habari za SiasaTangulizi

Polisi wampekua Zitto Kabwe nyumbani kwake

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini
Spread the love

IKIWA imepita siku moja tangu Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo , Zitto Kabwe kukamatwa na polisi jijini Dar es Salaam, leo Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni, limefanya upekuzi nyumbani kwake. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama cha ACT-Wazalendo na kuthibitishwa na Wakili wa Zitto, Jebra Kambole, inaeleza kuwa Mbunge huyo wa Kigoma Mjini aliwaongoza polisi hadi nyumbani kwake maeneo ya Masaki.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, baada ya polisi kukamilisha upekuzi, walimrudisha Zitto katika kituo cha Oysterbay na kwamba wakili wake anashughulikia suala la dhamana yake.

Kukamatwa kwa Zitto kumekuja siku kadhaa baada ya Jeshi la Polisi mkoani Kigoma kumtaka mwanasiasa huyo kujisalimisha polisi ili kuhojiwa kuhusu taarifa yake aliyoitoa Jumapili iliyopita, kuhusu mauaji ya askari na wananchi wa Kijiji cha Mpeta wilayani Uvinza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!