Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TTCL yathibitisha ‘kufyeka’ wafanyakazi 550
Habari MchanganyikoTangulizi

TTCL yathibitisha ‘kufyeka’ wafanyakazi 550

Spread the love

SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limethibitisha kutaka kupunguza wafanyakazi 550 kati ya 1,500 walioko nchi nzima, ambao hawana sifa za kitaalamu na kushindwa kuendana na kasi ya utendaji wa shirika hilo na serikali ya awamu ya tano. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na  TTCL hivi karibuni, inaeleza kuwa, zoezi la kupunguza wafanyakazi hao litatekelezwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma kwa kuzingatia misingi ya haki, uwazi, utu na maridhiano.

“Jambo hili si geni ndani ya shirika kwa kuwa mchakato wake ulianza mwanzoni mwa 2017, kwa majadiliano yaliyoshirikisha wafanyakazi kupitia vyama vyao, mamlaka za serikali na wadau wengine wa TTCL ambao mara zote wamekuwa wakijulishwa kwa ufasaha juu ya maendeleo ya zoezi hili,” inaeleza sehemu ya taarifa ya TTCL.

Aidha, taarifa hiyo inaeleza kuwa, TTCL inawasisitiza watumishi na wadau wote wa shirika hilo, kuendelea na utekelezaji wa majukumu yao kama kawaida hadi pale taarifa nyingine zitakapotolewa.

Taarifa ya TTCL imekuja baada ya baadhi ya vyombo vya habari kuripoti mpango wake wa kupunguza wafanyakazi kufuatia kauli iliyonukuliwa kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Omari Nundu wakati akielezea hatua za TTCL katika kukabiliana na mzigo mkubwa wa gharama za uendeshaji, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC).

Nundu aliieleza kamati hiyo ya bunge kuwa, idadi kubwa ya watumishi wa TTCL ni miongoni mwa sababu zinazochangia ukubwa wa gharama za uendeshaji wa shirika hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!