Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Nandy azindua Nandy Beauty Product
MichezoTangulizi

Nandy azindua Nandy Beauty Product

Nandy Beuty Product
Spread the love

KATIKA kuhakikisha anaunga juhudi za serikali ya viwanda na kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, Msanii wa muziki wa kizazi kipya Faustina Mfinanga ‘Nandy’ amezindua rasmi bidhaa zake za mafuta ya kupaka na sabuni za kuogea. Anaripoti Moses Mseti, Mwanza … (endelea).

Msani huyo anayetamba kwa sasa na kibao chake cha Ninogeshe, amewaambia waandishi wa habari jijini Mwanza leo kuwa lengo la kuleta bidhaa hizo sokoni ni kutimiza ndoto yake aliyokuwa nayo tangu utotoni.

Nandy ambaye ni kati ya wasanii wanawake wanaofanya vizuri kwa kuimba nyimbo laini zenye mashairi ya kuelimisha, amesema pamoja na kutimiza ndoto yake aliyokuwa nayo ya kuwa mfanyabiashara mkubwa pia bidhaa hizo zitachangia kukuza pato la taifa.

Pia alisema kuwa kwa muda mrefu mashabiki wake walikuwa wakimuuliza na kutamani kuona bidhaa zake na kwamba sasa amekata kiu yao kwa kuleta bidhaa hizo bora aina ya Nandy Beuty Soap na Nandy beuty Jelly zenye manukato mazuri.

Nandy ambaye alianza kuchomoza kwenye muziki wa kizazi kipya mwaka 2016, amesema kuingiza sokoni bidhaa zake itasaidia pia kuongeza ajira kwa vijana huku akiwaomba mashabiki zake kusapoti kwa kununua bidhaa hizo.

“Bidhaa hizi za mafuta ya kupaka na sabuni siyo kwa wanawake pekee ni kwa ajili watu wote na kwa lika zote na bidhaa hizi zinapatikana kote nchini,” alisema Nandy.

Mkurugenzi wa kampuni ya Grace Product, Pastasesa Kasisi, ambao ndiyo watengenezaji wa bidhaa hizo, alisema msanii huyo aliwafuata na kuwaeleza juu ya ndoto zake za kuwa mfanyabiashara mkubwa jambo ambalo waliamua kuungana na kutengeneza bidhaa hizo.

Kasisi amesema bidhaa hizo zinazotengenezwa na kampuni yao ni za asili na hazina madhara kwa watumiaji kwani zimetengenezwa na mimea ambayo ni mizuri kwa kiwango cha kimataifa.

Mmoja wa wasambazaji maarufu Kanda ya Ziwa wa bidhaa za Grace Product, Mayalla Zakaria amesema bidhaa hizo zitakuwa zinapatikana katika maduka yote ya jumla na rejareja katika mikoa yote huku akidai bei ya bidhaa hizo ni za kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!