Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto awavaa Polisi mapigano ya Kigoma
Habari za SiasaTangulizi

Zitto awavaa Polisi mapigano ya Kigoma

Spread the love

ZITTO Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), amelitaka Jeshi la Polisi Tanzania kutoa taarifa ya kina kuhusu tukio la mapigano kati ya askari na wananchi jamii ya Wanyantuzu wilayani Uvinza mkoani Kigoma. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tukio hilo lililotokea takribani siku 10 zilizopita, ambapo inadaiwa askari wawili kufariki dunia huku idadi ya wananchi waliopoteza maisha ikiwa haijulikani.

Kiongozi huyo ameetoa kauli hiyo leo Jumapili Oktoba 28, 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho Kijitonyama, Dar es Salaam.

Zitto ameomba idadi ya waliopoteza maisha katika tukio hilo kuwekwa wazi.

“Viongozi walikwenda eneo la tukio tunataka waseme, si tu kupata taarifa ya polisi bali tupate na sauti za wananchi juu ya kitu kilichotokea huko,” amesema Zitto.

“Tunahitaji kupata taarifa kamili ni wangapi walijeruhiwa, waliopoteza maisha kwa sababu wale ni Watanzania na wana haki ya kupewa ulinzi na kuishi sehemu yoyote.”

Amesema kama walifanya makosa kwa kuvamia eneo ambalo halitakiwi kufanyika shughuli za binadamu kuna taratibu za kufuata na si watu kuuawa.

“Vyombo vya habari havitoi taarifa kwa sababu wenye taarifa hawazitoi kwa wanahabari. Jana tulipata taarifa watu wanne walikwenda kupatiwa matibabu katika kituo cha afya cha Nguruka jambo hili ni baya na linatakiwa kukemewa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!