Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Skauti sasa kutua Vyuo Vikuu
Habari za Siasa

Skauti sasa kutua Vyuo Vikuu

Mwantumu Mahiza, Skauti Mkuu wa Chama cha Maskauti Tanzania
Spread the love

BAADA ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Skauti Mkuu wa Chama cha Maskauti Tanzania, Mwantumu Mahiza ameahidi kuieneza skauti katika vyuo vya kati na vyuo vikuu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Mahiza ameyaahidi hayo leo tarehe 3 Oktoba 2018 ikulu jijini Dar es Salaam, ambapo alimhakikishia Rais John Magufuli kwamba atautumia vyema wadhifa huo katika kujenga maadili ya vijana wa kitanzania.

Mahiza ameeleza kuwa, kwa miaka mingi skauti ilienea katika shule za msingi na sekondari na kwamba ni wakati husika kwa taasisi hiyo ya kujenga maadili ya vijana wa Tanzania kuenea katika vyuo vyote hapa nchini.

“Nakushukuru kwa kuniteua kulea vijana wa Tanzania kupitia skauti, wajibu wangu ni mambo mawili, kuhakikisha skauti inaenea katika vyuo vya kati na vyuo vikuu kwa sababu miaka mingi ilienea shule za msingi na sekondari,” amesema Mahiza.

Katika hatua nyingine, Mahiza aliahidi kufanikisha ujenzi wa kambi ya kimataifa ya Skauti jijini Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!