Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wawashikilia watu 68 kwa kuharibu miundombinu
Habari Mchanganyiko

Polisi wawashikilia watu 68 kwa kuharibu miundombinu

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP Ulrich Matei
Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu 68 kwa tuhuma za kufanya uharibifu wa miundombinu ya maji katika Kijiji cha Ngole kilichopo Kata ya Ilungu, Tarafa ya Tembela, Wilaya ya Mbeya Vijijini. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 18 Agosti, 2018 na SACP Ulrich Matei, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya.

Kamanda Matei amesema watuhumiwa hao ambao wanaume wako 62 na wanawake 8, katika msako mkali uliofanywa na polisi tarehe 17 Agosti, 2018 katika Kijiji cha Ngole.

“Awali mnamo tarehe 14 Agosti mwaka huu kuanzia majira ya saa 10:00 asubuhi huko katika Kijiji cha Ngole, watuhumiwa hao kwa makusudi na bila uhalali waliharibu mabomba na vyanzo vya maji kwa kutumia silaha za jadi na kusababisha hasara ya takribani Sh. 14 milioni, mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni michango ya baadhi ya wanakijiji na wafadhili,” amesema Kamanda Matei.

Kamanda Matei amesema watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

error: Content is protected !!