Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Michezo Magufuli, Kikwete wamuaga Mzee Majuto Karimjee
MichezoTangulizi

Magufuli, Kikwete wamuaga Mzee Majuto Karimjee

Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli na Rais mstaafu Jakaya Kikwete amewaongoza mamia ya watanzania kuaga mwili wa marehemu muigizaji wa vichekesho Amri Athumani ‘Mzee Majuto” kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mwili wa Mzee Majuto uliwasili Ukumbini hapo saa nane na shughuli ya kuaga ikaanza ikiwemo salamu za rambirambi na dua ya kuombea iliongozwa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum.

Viongozi mbalimbali wa Serikali, vyama vya siasa na vya kijamii na viongozi wa dini wameungana na waigizaji wenzake na marehemu pamoja na wananchi kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu.

Mwili wa Mzee Majuto ulitolewa kwenye Monchwari ya Muhimbili saa 5 asubuhi na kupelekwa kwenye msikiti wa Maamul Upanga kwa ajili ya kuswaliwa na baadaye saa nane mchana Mwili uliwasilishwa kwenye viwanja vya Kareem Jee kwa ajili ya kuagwa.

Taswira ya Viwanja hivyo ilikuwa imefurika wasanii mbalimbali wa maigizo wakiwamo Jacob Steven JB, Cloud 112, Joti, Dr. Cheni, Haji Manara na wengine wengi.

Pia kulikuwepo watu mbalimbali mashuhuri kama Humphery Polepole, Naibu waziri wa Habari Vijana, Sanaa na michezo Juliana Shoza.

Majira ya saa 9 aliwasili Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakari Bin Zuberi na baadaye aliingia Rais wa Tanzania John Magufuli.

Wakati huo huo vikindi mbalimbali vilitoa salaam za rambirambi pamoja kuuaga Marehemu Mzee Majuto.

Mzee Majuto aliaga dunia usiku wa kuamkia jana katika Hospitali ya taifa Muhimbili jijini dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!