Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kampuni ya Ulinzi wamwita Waziri Mhagama
Habari Mchanganyiko

Kampuni ya Ulinzi wamwita Waziri Mhagama

Spread the love

WAFANYAKAZI wa kampuni ya ulinzi ya Tele Security Campan Ltd wamemuomba Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama kuingila kati mgogoro uliopo kati ya wafanyakazi hao na kampuni kutokana na fedha zao kutoingizwa katika mfuko wa jamii NSSF. Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Wafanyakazi hao wakizungumza na vyombo vya ulinzi walisema kuwa kampuni hiyo imekuwa ikiwakata fedha zao kwa madai kuwa wanaingiza katika mfuko wa jamii lakini fedha hizo hazipelekwe kama inavyotakiwa.

Hata hivyo walisema kuwa viongozi wa kampuni hiyo wamekuwa wakiwafukuza kazi wafanyakazi ambao wamekuwa wakionesha nguvu ya ushawishi wa kudai pesa zao kwa ajili ya mafao.

Mmoja wa wafanyakazi ambaye alijitambulisha kwa jina la Mlugu Chilewa alisema kuwa tangu mwaka 2011 hadi sasa.

Chilewa alisema kuwa katika mwaka 2011 kampuni ilikuwa ikiwakata sh.11500 kwa ajili ya NSSF na ilipofika mwaka 2016 mwezi wa pili walikanza kukatwa kiasi cha sh 11700 ambazo nazo haziingizwi NSSF.

Naye Ruzoya Julius alisema kuwa kampuni hiyo imekuwa ikiwatishia kuwafukuza kazi au pale wanapokuwa wakidai mafao yao.

Aidha alisema kuwa wafanyakazi wa kampui hiyo wanapoendelea kudai makato yao yapelekwe kwenye mifuko ya jamii wanaambiwa waandike barua ya kuacha kazi ndipo waweze mafao yao yawee kupelekwa kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii.

Kutokana na hali hiyo wamekuomba Waziri mwenye dhamana Jenistara Mhagama kuingilia kati ili kuweza kutatua hali hiyo kwani inawafanya wafanyakazi wa kampuni hiyo kuishi Maisha magumu na yenye wasiwasi.

Mbali nahilo walisema pamoja na kukatwa hela hizo bado kampuni haipeleki makato NSSF na kampuni haichangii fedha kama inavyotakiwa kisheria.

Alipoulizwa Meneja wa Kampuni hiyo kanda ya Dodoma Fidelisi Luhunga kuhusu malalamiko hayo alisema kuwa yeye siyo msemaji wa kampuni ila msemaji mkuu ni meneja wa Kampuni ambaye yupo Jijini Dae es Salaam.

Hata hivyo alisema yupo mtu mmoja ambaye anakusanya fedha zote kwa ajili ya kuziingiza katika Mfuko wa Hifadhi ya Jamii.

Alipotafutwa Mkurugenzi mkuu ambaye alijitambuliwa kwa jina moja la Mkeni kwa ajili ya kutoa ufafanuzi juu ya malalamiko hayo alisema kuwa yeye awezi kusema lolote wenye majibu ni NSSF.

Hata hivyo NSSF walithibitisha kuwa wafanyakazi wa kampuni hiyo hawana fedha yoyote na majina yao hayapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!