Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo CAF yawatoa kifungoni waamuzi wa Tanzania
Michezo

CAF yawatoa kifungoni waamuzi wa Tanzania

John Komba, mwamuzi wa Tanzania mwenye beji ya Fifa
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Africa (CAF) limetoa majibu ya uchunguzi wa waamuzi wanne wa Tanzania waliofikishwa kwenye Shirikisho hilo kufuatia kuripotiwa kwa vurugu kwenye hoteli waliyofikia nchini Burundi walipokwenda kuchezesha mechi ya Ligi ya Mabingwa Africa Kati ya Rayon ya Rwanda na Lydia Ludica kutoka nchini Burundi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Waamuzi hao ambao ni Soud Idd Lila, Frank John Komba, Mfaume Ali Nasoro na Israel Mujuni walikuwa katika hali ya sintofahamu baada ya kuibuka kwa vurugu kubwa katika hoteli waliofikia kutokana ya madai ya kuwa moja ya timu hizo mbili ilitaka kupanga matokeo kupitia waamuzi hao.

Taarifa iliyotolewa na shirikisho la mpira wa miguu nchni TFF, ilisema CAF, kupitia Katibu wake Mkuu Amr Fahmy ilijilidhisha kuwa hakuna jambo lolote baya lililowazunguka waamuzi hao kuhusiana na mchezo huo uliochezwa tarehe 21 Februari, 2018 katika dimba la Prince Louis Rwagasore, Burundi. Na hivyo wapo safi kuendelea na majukumu yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!