Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif aichamba CCM
Habari za Siasa

Maalim Seif aichamba CCM

Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa CUF. Picha ndogo Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) amesema kuwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM) sio chama cha kukimbilia.  Anaripoti Regina Kelvin …(endelea).

Amesema, haoni sababu mtu mwenye msimamo imara kukimbilia kwenye chama hicho na kwamba, mfumo wa uendeshaji wake haukidhi wara kuridhisha.

“Siridhishwi hata kidogo na utendaji wa CCM” amesema Maalim Seif alipokuwa Kilimahewa visiwani Zanzibar wakati akizindua Jumuiya ya Wazee wa chama hicho (JUZECUF) jana.

Amesema kuwa, hana ndoto ya kujiunga na CCM ambayo utendaji wala mwelekeo wake kwa taifa hauelewiki.

Maalim Seif ameeleza kuwa, kinachotokea katika serikali inayoindwa na CCM hasa kukamatakamata hovyo hakijawahi kutokea hata wakati wa Ukoloni.

“CCM inatakiwa kuelewa haiwezi kutawala nje ya mfumo ambao Watanzania wanavyotaka nchi yao itawaliwe,” amesema na kuongeza;

“Mara kwa mara unasikia diwani ama mbunge kaingia CCM, tena kwa kutoa tamko maalumu. Haya mliyaona wapi?” amehoji Malim Seif.

“Imefika hatua sasa Mwenyekiti wa Kijiji kwa kuwa tu anatoka CCM basi anaweza kuamrisha Jeshi la Polisi likukamate na unakamatwa kweli na kuwekwa ndani,”amesema Maalim Seif.

Katika mazungumzo na wazee hao Maalim Seif amegawa kadi kwa wanchama wapya huku akiahidi kuendelea kuimarisha chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!