MAALIM Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) amesema kuwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM) sio chama cha kukimbilia. Anaripoti Regina Kelvin …(endelea).
Amesema, haoni sababu mtu mwenye msimamo imara kukimbilia kwenye chama hicho na kwamba, mfumo wa uendeshaji wake haukidhi wara kuridhisha.
“Siridhishwi hata kidogo na utendaji wa CCM” amesema Maalim Seif alipokuwa Kilimahewa visiwani Zanzibar wakati akizindua Jumuiya ya Wazee wa chama hicho (JUZECUF) jana.
Amesema kuwa, hana ndoto ya kujiunga na CCM ambayo utendaji wala mwelekeo wake kwa taifa hauelewiki.
Maalim Seif ameeleza kuwa, kinachotokea katika serikali inayoindwa na CCM hasa kukamatakamata hovyo hakijawahi kutokea hata wakati wa Ukoloni.
“CCM inatakiwa kuelewa haiwezi kutawala nje ya mfumo ambao Watanzania wanavyotaka nchi yao itawaliwe,” amesema na kuongeza;
“Mara kwa mara unasikia diwani ama mbunge kaingia CCM, tena kwa kutoa tamko maalumu. Haya mliyaona wapi?” amehoji Malim Seif.
“Imefika hatua sasa Mwenyekiti wa Kijiji kwa kuwa tu anatoka CCM basi anaweza kuamrisha Jeshi la Polisi likukamate na unakamatwa kweli na kuwekwa ndani,”amesema Maalim Seif.
Katika mazungumzo na wazee hao Maalim Seif amegawa kadi kwa wanchama wapya huku akiahidi kuendelea kuimarisha chama hicho.
Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...
By Regina MkondeMay 2, 2024Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...
By Mwandishi WetuMay 2, 2024Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...
By Gabriel MushiApril 30, 2024Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...
By Gabriel MushiApril 30, 2024
Leave a comment