Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yamgeuka Lugola Buyungu
Habari za Siasa

CCM yamgeuka Lugola Buyungu

Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM. Picha ndogo Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani
Spread the love

MAZINGIRA ya Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Buyungu yamekilazimisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumtosa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Ni kile kinachoelezwa kuwasakama vijana wa bodaboda na kudai ‘dawa yao inachemka’ ambapo Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Bashiru Ally amesema, Lugola anapaswa kuanza kwanza kutafakari utendaji wa Jeshi la Polisi.

CCM na vyama vingine vya upinzani vinaendelea na kampeni zake kwenye jimbo hilo ambapo uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Agosti 12 mwaka huu.

Juzi akiwa wilayani Kakongo lilipo Jimbo la Buyungu ndani ya Mkoa wa Kigoma Dk. Bashiru amesema, polisi wamekuwa wakikamata bodaboda na kuzijaza kwenye vituo vya polisi kwa kile alichoeleza kutokuwepo kwa sababu za msingi.

Kiongozi huyo wa CCM amesema, lazima Lugola na timu yake wahakikishe wanakomesha vitendo vya kunyanyasa waendesha bodaboda.

Ameeleza zaidi kuwa, Jeshi la Polisi linapaswa kutenda haki na kuzingatia utu wa watu kwa kuwa, baadhi ya maeneo malalamiko ya kunyanyaswa yanajitokeza.

Dk. Bashiru ameeleza kuwa, hawako tayari kuwatetea bodaboda lakini kuna kila sababu ya Jeshi la Polisi kuata na kusimamia haki na si kuwanyanyasa vijana hao wa bodaboda.

“Hatuwatetei bodaboda…nataka Waziri wa Mambo ya Ndani kufanyia kazi suala hilo…” ameeleza Dk. Bashiru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!