Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yamgeuka Lugola Buyungu
Habari za Siasa

CCM yamgeuka Lugola Buyungu

Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM. Picha ndogo Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani
Spread the love

MAZINGIRA ya Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Buyungu yamekilazimisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumtosa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Ni kile kinachoelezwa kuwasakama vijana wa bodaboda na kudai ‘dawa yao inachemka’ ambapo Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Bashiru Ally amesema, Lugola anapaswa kuanza kwanza kutafakari utendaji wa Jeshi la Polisi.

CCM na vyama vingine vya upinzani vinaendelea na kampeni zake kwenye jimbo hilo ambapo uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Agosti 12 mwaka huu.

Juzi akiwa wilayani Kakongo lilipo Jimbo la Buyungu ndani ya Mkoa wa Kigoma Dk. Bashiru amesema, polisi wamekuwa wakikamata bodaboda na kuzijaza kwenye vituo vya polisi kwa kile alichoeleza kutokuwepo kwa sababu za msingi.

Kiongozi huyo wa CCM amesema, lazima Lugola na timu yake wahakikishe wanakomesha vitendo vya kunyanyasa waendesha bodaboda.

Ameeleza zaidi kuwa, Jeshi la Polisi linapaswa kutenda haki na kuzingatia utu wa watu kwa kuwa, baadhi ya maeneo malalamiko ya kunyanyaswa yanajitokeza.

Dk. Bashiru ameeleza kuwa, hawako tayari kuwatetea bodaboda lakini kuna kila sababu ya Jeshi la Polisi kuata na kusimamia haki na si kuwanyanyasa vijana hao wa bodaboda.

“Hatuwatetei bodaboda…nataka Waziri wa Mambo ya Ndani kufanyia kazi suala hilo…” ameeleza Dk. Bashiru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!